Psalms 65:9-13


9 aWaitunza nchi na kuinyeshea,
waitajirisha kwa wingi.
Vijito vya Mungu vimejaa maji
ili kuwapa watu nafaka,
kwa maana wewe umeviamuru.

10 bUmeilowesha mifereji yake
na kusawazisha kingo zake;
umeilainisha kwa manyunyu
na kuibariki mimea yake.

11 cUmeuvika mwaka taji ya baraka,
magari yako yanafurika kwa wingi.

12 dMbuga za majani za jangwani umezineemesha;
vilima vimevikwa furaha.

13 ePenye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama,
na mabonde yamepambwa kwa mavuno;
vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.
Copyright information for SwhKC